Search This Blog

Thursday, December 31, 2020

Rouhani amfananisha Trump na Saddam Hussein


Rais wa Iran Hassan Rouhani, amemfananisha Rais wa Marekani Donald Trump na kiongozi wa zamani wa Iraq aliyepinduliwa Saddam Hussein.

"Saddam alitupiga vita kwa miaka 8 na mwishowe aliangamizwa. Trump alituwekea vita vya miaka 3 vya kiuchumi, na atamaliza kuhudumu wiki chache zijazo. Atakumbukwa kama mtu asiye na heshima katika historia.’’

Rouhani, ambaye alishiriki katika hafla ya ufunguzi wa miradi kadhaa katika mkoa wa Magharibi ya Azerbaijan wa Iran kwa njia ya video, alifanya tathmini juu ya shambulizi la Marekani ambalo Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi Qasim Soleimani aliuawa pamoja na sera ya Trump nchini humo.

Akisisitiza kwamba Trump amefanya mauaji mengi yasiyosahaulika kama vile ya Kamanda wa Kikosi cha Jerusalemu Soleimani na Rais wa Hashdi Shabi Mhandisi Abu Mahdi, ambayo yatalipiza kisasi, Rouhani alisema,

"Trump amefanya unyama mwingi. Mojawapo ya matendo yake yasiyosameheka ni mauaji ya Soleimani na Mhandisi. Hii imetuletea maumivu na uchungu ndani ya mioyo yetu. Watu wa eneo hilo na wananchi wa Iran watalipiza kisasi kwa wakati unaofaa. Adui hakika ataumia katika harakati hizi mbaya za mauaji ya kinyama. Watu wa Iran watachukua msimamo mkali katika hatua ya upinzani. Watu wote wameelewa kuwa maadamu Marekani iko katika eneo hili, hawatafikia malengo yao ya furaha zinazotarajiwa. Njia na mwelekeo wa Soleimani utaendelea."

Katika hotuba yake ya maelezo, Rouhani pia aligusia siasa za ndani ya nchi.  

Akijibu kukosolewa kwa serikali ya ndani, Rouhani alisema,

"Wale wanaosema wanapingana na Marekani na kudhoofisha serikali wanadanganya. Serikali iko kwenye uwanja wa vita. Wale wanaodhoofisha serikali ni wafuasi na waliokuwa upande wa Marekani."




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...