Search This Blog

Thursday, December 31, 2020

Ronaldo bado yupo yupo japo umri umekwenda


Mshambuliaji wa Juventus, Cristiano Ronaldo amesema hana mpango wa kustaafu soka hivyo ataendelea kucheza kwa miaka mingi zaidi licha ya kukaribia umri wa miaka 36.

Ronaldo raia wa Ureno msimu wa 2020/21 ametupia kambani magoli 16 kwenye mechi 14 alizocheza katika mashindano yote, huku 12 akifunga kwenye ligi ya Serie A.

Ronaldo atakuwa na umri wa miaka 36 ifikapo mwezi Februari 2021 ana mkataba na timu ya Juventus hadi ifikapo mwaka 2021 na amesema anataka kusakata kabumbu hadi akitimiza umri wa miaka 40.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...