Search This Blog

Friday, December 18, 2020

Robert Lewandowski ashinda tuzo ya mwanasoka bora wa Fifa


 Robert Lewandowski , msahambuliaji nyota wa Bayern Munich alishinda tuzo ya mwanasoka bora wa Fifa huko Zurich na kuwashinda washindi wa miaka iliyotangulia ,Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.

Mshambuliaji huyo kutoka Poland alifunga mabao 55 katika michezo 47 tu msimu uliopita na kuisaidia miamba ya Ujerumani Bayern Munich kunyakua mataji 3 katika msimu moja,yaani kombe la ligi ya Ujerumani,kombe la taifa na ligi ya mabingwa ulaya.

Lewandowski mwenye umri wa miaka 32, alimaliza msimu akiwa mfungaji bora wa ligi, kombe la taifa na Ligi ya Mabingwa.

Mlinzi wa Manchester City Lucy Bronze alishinda tuzo ya mchezaji bora wa wanawake.

Washindi waliamuliwa na uteuzi kutoka kwa manahodha wa timu za mataifa na makocha wakuu, kura ya mtandaoni ya mashabiki na wawakilishi 200 wa vyombo vya habari.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...