Search This Blog

Sunday, December 20, 2020

RC Byakanwa amewataka watendaji kata Mahurunga,Tangazo,Dihimba kuwaorodhesha vijana wote ambao hawajulikani walipo


Na Faruku Ngonyani, Mtwara.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gellasius Byakanwa amewataka wananchi wanaishi kata za Mahurunga ,Tangazo na Dihimba Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara kuimarisha ulinzi na usalama katika maeneo yao.

Ameyazungumza hayo alipofanya ziara kwa katika kata hizo kuzungumza na kutoa elimu kwa  wakulima juu ya namna bora ya kuongeza uzalishaji wa mazao mbalimbali katika maeneo yao.

RC Byanakwa amesema kuwa wapo baadhi ya wananchi wamekuwa na tabia ya kuwahifadhi waharifu majumbani kwao hali inayopelekea kuhatarisha amani kwa kata hizo.

Mkuu huyo wa Mkoa amechukua fursa kuwaagiza watendaji kata wa kata hizo kuhakikisha wanawaorodhesha vijana wote  ambao hawajulikani walipo na wanafanya nini.

“Taarifa tulizonazo wanamtwara wote mnaokaa kwenye mipaka hii mnaficha uhalifu hamtoi taarifa za watu wanaojihusisha na uhalifu,sasa wale wenye watoto ambao hawajulikani  wako wapi na wanafanya nini,nataka watendaji kata kuwaorodhesha vijana wote ambao hawajulkani walipo”Byakanwa.  

Kwa sasa Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa vyombo vya ulinzi na usalama tayari vimeimarisha ulinzi katika maeneo hayo huku akitoa wito kwa wananch kuendelea kuwafichua waharifu ili waweze kushughulikiwa.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...