Search This Blog

Wednesday, December 23, 2020

Rais Magufuli afanya uteuzi wa Kamishna wa Maadili


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Sivangilwa Sikalalilwa Mwangesi (Jaji wa Mahakama ya Rufani) kuwa Kamishna wa Maadili.

Mwangesi ameteuliwa kushika wadhifa huo baada ya Jaji wa Mahakama ya Rufani Mstaafu Harold Nsekela kufariki dunia.

Uteuzi wa Mwangesi unaanza leo tarehe 23 Desemba, 2020 na ataapishwa kesho tarehe 24 Desemba, 2020 saa 4:00 asubuhi, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...