Search This Blog

Sunday, December 6, 2020

Raia wa Ubelgiji waandamana kupinga ubaguzi na shinikizo za polisi


Maandamano ya kupinga ubaguzi na shinikizo za polisi yaliandaliwa katika mji mkuu wa Brussels nchini Ubelgiji.

Takriban watu 150 walikusanyika katika mji mkuu wa Brussels kwa ajili ya maandamano ya kupinga ubaguzi na shinikizo za polisi.

Waandamanaji walikusanyika mbele ya jengo la baraza la Jumuiya ya Ulaya (EU) wakiwa wamebeba mabango na kutoa kaulimbiu dhidi ya ubaguzi.

Waandamanaji hao waliopinga shinikizo za polisi zilizoongezeka Ubelgiji na Ufaransa, pia walikosoa mazungumzo ya kanuni mpya ya usalama huku wakitoa wito wa kujiuzulu kwa Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron. 

Maafisa wa polisi walishika doria na kuchukuwa hatua kali za kiusalama katika barabara zinazoelekea kwenye eneo la maandamano. 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...