Mchezo kati ya Paris St-Germain dhidi ya Istanbul Basaksehir utachezwa siku ya Jumatano baada ya kutelekezwa siku ya Jumanne wakati afisa wa mechi hiyo akishutumiwa kutoa maneno ya kibaguzi .
Instanbul imedai mwamuzi wa nne Sebastian Coltescu alitumia lugha ya kibaguzi kwa kocha wao msaidizi Pierre Webo.
Mchezaji wa zamani wa timu ya taifa, Webo alioneshwa kadi nyekundu baada ya kurushiana maneno na muamuzi wa nne
Wachezaji wa Instambul walitoka nje ya uwanja wakikemea kitendo hicho, huku PSG wakifuatia
Tukio hilo lilitokea dakika 14 tu tangu kuanza kwa mchezo wa kundi H, mchezo ambao walikuwa hawajafungana.
Mchezo huo utaanza Jumanne kuanzia dakika ya 14 ya mchezo,mchezo utaanza saa 2:55 saa za Afrika Mashariki
Maafisa wengine watausimamia mchezo huo, huku Mholanzi Danny Makkelie akiteuliwa kuwa mwamuzi.

No comments:
Post a Comment