Search This Blog

Saturday, December 5, 2020

Matokeo ya uchaguzi wa Georgia yatangazwa


Chama tawala cha Georgian Dream kimethibitishwa kushinda uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Georgia mnamo Oktoba 31.

Tume ya Kuu ya Uchaguzi ilitangaza matokeo ya mwisho ya uchaguzi huo uliofanyika.

Kwa mujibu wa matokeo hayo, chama tawala cha Georgian Dream kilishinda viti 90 wabunge kati ya 150. Hivyo basi, chama tawala kitaweza kuunda serikali peke yake.

Vyama vingine vilivyoshirikia uchaguzi vilipata idadi ya viti bungeni kama ifuatavyo; Chama cha Strength is in Unity viti 36, Chama cha Giorgi Vaşadze - Agmaşenebeli viti 4, Georgia European Party 5, Patriots Alliance Party viti 4, Georgia Workers Party kiti 1, Alekoashvili - Citizens Party viti 2, Chama cha Cone viti 4, na Chama cha Lelo viti 4.

Vyama vya upinzani, ambavyo havikubaliani na matokeo ya uchaguzi na kutaka uchaguzi huo urudiwe tena upya, vimefanya maandamano kote nchini mara kadhaa tangu Oktoba 31.

Serikali imeweka wazi uamuzi wake wa kutorudia uchaguzi huo kwa mara nyingine.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...