Search This Blog

Friday, December 11, 2020

Marekani yarudisha maeneo ya kijeshi kwa Korea Kusini


Kikosi cha jeshi la Marekani kimerudisha maeneo 12 ya kijeshi yaliyoko nchini Korea Kusini kwa wamiliki.

Kulingana na taarifa za shirika la habari la Korea Kusini YONHAP, iliarifiwa kuwa maafisa wa nchi hizo mbili walikubaliana kwamba Kikosi cha Kimarekani na Kikorea (USFK) kitakabidhi maeneo ya kijeshi yaliyoko kwenye baadhi ya ngome ya Yongsan katika mji mkuu wa Seoul.

Mbali na ardhi mbili za ngome ya Yongsan, kambi ya Camp Kim iliyoko katika mji mkuu pamoja na maeneo 4 ya kijeshi, Camp Walker iliyoko mjini Daegu, uwanja wa golf mjini Hanam, kituo cha Jeshi la Wanamaji la Marekani mjini Pohang na eneo la mazoezi ya risasi lililoko Taebaek pia yalirudishwa kwa Korea Kusini.

Pande zote ziliafikiana kwa makubaliano juu ya mashauriano na kugawana gharama za kusafisha mazingira, pamoja na taratibu zinazofaa kufuatwa.

Nchi ya Korea Kusini ambayo iliungwa mkono na Umoja wa Mataifa (UN) katika suala la muungano ikiongozwa na Marekani katika Vita vya Korea vya mwaka 1950-1953, ina wanajeshi 28,500 wa Marekani wanaohudumu.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...