Search This Blog

Tuesday, December 1, 2020

Mali za Ushirika kuendelea kurejeshwa


Serikali imesisitiza kuendelea kurejesha mali zote za vyama vya ushirika, zilizochukuliwa kwa hila na wizi, ambapo hadi sasa mali 59 zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 68 na milioni 900 zimerejeshwa kwenye vyama hivyo.

Msisitizo huo wa serikali, umetolewa jijini Dodoma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Bw. Gerald Kusaya, wakati alipokuwa akifungua kongamano la uwekezaji wa Benki ya Kilimanjaro Co-operative Bank Limited (KCBL).

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Anna Mghwira, ambaye ndiye aliyefanya juhudi za kuhakikisha benki ya (KCBL) inafufuka, ameweka bayana malengo na ndoto walizonazo kuwa na benki ya taifa ya ushirika.

Nao wawekezaji wa benki ya (KCBL), benki ya CRDB na Kilimanjaro Development Forum (KDF), wakawataka wanaushirika kuikimbilia benki hiyo kwa kununua hisa, kwani ushirika ndio silaha kubwa kwenye maendeleo.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...