Magaidi 9 wa kundi la Boko Haram wameangamizwa katika operesheni dhidi yao nchini Nigeria.
Naibu Msemaji wa Wizara ya Ulinzi Bernard Onyeuko ametangaza kuwa jeshi lilifanya operesheni dhidi ya kundi la kigaidi la Boko Haram katika jimbo la Borno.
Akibainisha kuwa wanachama 9 wa kundi hilo wameuawa katika operesheni hiyo, Onyeuko ameripoti kuwa wengi wao walikimbia wakiwa wamejeruhiwa.
Ngome za magaidi hao zimeangamizwa na idadi kubwa ya risasi pamoja na magari mawili ya silaha vimekamatwa.

No comments:
Post a Comment