Search This Blog

Sunday, December 20, 2020

Jeshi la Nigeria lawaua Magaidi 9 wa kundi la Boko Haram


Magaidi 9 wa kundi la Boko Haram wameangamizwa katika operesheni dhidi yao nchini Nigeria.

Naibu Msemaji wa Wizara ya Ulinzi Bernard Onyeuko ametangaza kuwa jeshi lilifanya operesheni dhidi ya kundi la kigaidi la Boko Haram katika jimbo la Borno.

Akibainisha kuwa wanachama 9 wa kundi hilo wameuawa katika operesheni hiyo, Onyeuko ameripoti kuwa wengi wao walikimbia wakiwa wamejeruhiwa.

Ngome za magaidi hao zimeangamizwa na idadi kubwa ya risasi pamoja na magari mawili ya silaha vimekamatwa.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...