Search This Blog

Thursday, December 10, 2020

Godbless Lema na familia yake wapata hifadhi Canada


Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, amepata nafasi ya hifadhi ya kisiasa nchini Canada.

Taarifa kutoka nchini Kenya zinasema, Lema ameondoka jana nchini humo akiwa na familia yake, Wakili wake George Luchiri Wajackoyah amethibitisha.

Mwezi uliopita Polisi nchini Kenya walimkamata kwa madai ya kuingia nchini humo kinyume na sheria na kumuachia huru baada ya muda mfupi.

Kwa mujibu wa Wakili wake, Wajackoyah, Lema ambaye alikua ameambatana na familia yake alikua akielekea jijini Nairobi kwa ajili ya kutafuta makazi ya muda baada ya kutishiwa maisha.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...