Waziri Mkuu wa Bahrain Khalifa bin Salman al-Khalifa ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 84.
Kulingana na taarifa zilizotolewa na vyanzo rasmi vya habari nchini Bahrain, iliripotiwa kuwa al-Khalifa alifariki katika hospitali aliyokuwa akipokea matibabu nchini Marekani.
Mamlaka kuu ya Kifalme ya Bahrain imetangaza kuwa mazishi ya Waziri Mkuu yatafanyika na kuhusisha washiriki wa familia pekee.

No comments:
Post a Comment