Zoezi la upigaji kura lilianza rasmi saa 06.00 za asubuhi katika uchaguzi huo unaoshindanisha wagombea 13 wa nafasi ya urais.
Rais wa awamu ya mwisho Roch Marc Christian Kabore ambaye ameahidi kuimarisha hali ya usalama nchini humo anatarajiwa kuhifadhi kiti chake cha urais kushinda tena uchaguzi huo.
Shughuli ya upigaji kura inatarajiwa kumalizika saa 18.00 za jioni. Endapo hakutakuwa na mgombea yeyote wa urais atakayefikisha asilimia 50 ya kura kwenye duru ya kwanza ya uchaguzi, wagombea wenye kura nyingi zaidi watapambana tena kwenye duru ya pili.
Takriban wananchi milioni 6.5 wameweza kusajiliwa kama wapiga kura katika nchi ya Burkina Faso.

No comments:
Post a Comment