Search This Blog

Thursday, November 26, 2020

Trump aonyesha ishara za kuwa tayari kuondoka Ikulu


Rais Donald Trump wa Marekani amesema ataondoka Ikulu ikiwa Joe Biden atathibitishwa rasmi kuwa rais anayefuata wa Marekani kwa kura za wajumbe.

Raia amekataa kukubali alishindwa katika uchaguzi uliofanyika Novemba 3 na kuwaambia wanahabari Alhamisi itakuwa vigumu kwake kukiri kushindwa.

Pia kwa mara nyingine tena amedai uchaguzi huo ulikumbwa na wizi wa kura. Bwana Biden anaongoza kura za wajumbe kwa kupata 306 huku Trump akiwa na kura 232.

Kura alizopata Bwana Biden zikiwa zimepita 270 idadi inayohitajika kwa mgombea kuwa rais wa Marekani.

Bwana Biden pia anaongoza kwa wingi wa kura kwa zaidi ya milioni 6.

Wawakilishi wa kura za wajumbe watakutana mwezi ujao kuidhinisha rasmi kura zilizopigwa huku Joe Biden wa chama cha Democratic akisubiri kuapishwa kuwa rais Januari 20.

Rais na wafuasi wake wamewasilisha kesi kadhaa wakipinga uchaguzi lakini nyingi zimetupiliwa mbali.

Mapema wiki hii, Bwana Trump hatimaye alikubali kuruhusu kuanza kwa mchakato wa kukabidhi madaraka kwa rais mteule Joe Biden baada ya wiki kadhaa za sintofahamu.

Uamuzi huo unamaanisha Bwana Biden anaweza kupata taarifa za usalama wa nchi na kuwasiliana na maafisa wa juu serikalini pamoja na kuweza kutumia mamilioni ya madola wakati anajitayarisha kuchukua rasmi madaraka Januari 20.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...