Search This Blog

Thursday, November 12, 2020

Rais Magufuli kufungua bunge leo


Rais wa nchi Tanzania John Magufuli hii leo atalihutubia taifa kupitia bunge la 12 na kulifungua rasmi huko katika mji mkuu wa Dodoma.

Watanzania kutoka maeneo mbalimbali ya nchi wanaisuburi kwa hamu hotuba ya rais ambayo inategemewa kutoa dira ya serikali baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwezi uliopita na kumpa ushindi wa asilimia 84.4 huku chama tawala kikijizolea ushindi wa wabunge kwa zaidi ya asilimia tisini.

Hata hivyo, mpaka sasa baadhi ya vyama vya upinzani nchini humo hawajakubali matokeo ya Uchaguzi uliopita kwa madai uligubikwa na mazingira ambayo hayakuwa huru.

Tuhuma hizo zimetupiliwa mbali na Tume ya Taifa ya Uchaguzi



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...