Vyanzo vya kiintelijensia vya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo vimethibitisha kuwa mwanamuziki maarufu nchini humo Tshala Muana amekamatwa.
Hadi kufikia sasa familia ya msanii huyo bado haijatoa taarifa yoyote lakini vyanzo vya habari nchini humo vinasema kwamba alikamatwa hapo jana majira ya mchana.
Hivi karibuni mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 62 ametoa wimbo kwa jina, 'kukosa shukrani' ambao inaaminika kuwa ndio chanzo cha masaibu yake.
Mashairi ya wimbo huo yanaashiria mtu ambaye hakutajwa kwa jina alipewa mazingira mazuri yakumuwezesha maishani lakini amesahau kurejesha wema baada ya kuingia madarakani.
Wengi wanaamini kuwa mwanamuziki huyo ambaye ni mshindi wa tuzo mbalimbali anamzungumzia rais Felix Tshisekedi -lakini Tshala Muana bado hajathibitisha hilo.
Tshala Muana alikuwa karibu sana na familia ya aliyekuwa rais wa Congo Joseph Kabila.

No comments:
Post a Comment