Siku chache baada ya mbunge wa Jimbo la Nzega mkoani Tabora ambaye pia ni mwanachama wa klabu ya Simba, Dk. Hamisi Kigwangalla kumuomba radhi mwekezaji wa klabu ya Simba, mfanyabiashara Mohammed Dewji maarufu Mo Dewji hatimaye Mo aye ameonyesha busara yake kwa kupokea msamaha huo.
Kupitia ukurasa wake wa istagramu Mo Dewji amesema amemsamehe kwai wote walikuwa a mapenzi ya dhati na simba.
Kwenye instagramu yake Mo ameandika hivi;
Nia njema ni tabibu, nia njema ni ibada. Sote tuna mapenzi ya dhati na Simba, hata tulipokwazana ilikua katika nia njema kwenye maendeleo ya timu yetu. Naomba radhi nilipokosea na mimi uliponikosea nishasamehe. Tuijenge Simba pamoja sasa 💪🏾 #NguvuMoja

No comments:
Post a Comment