Search This Blog

Sunday, November 15, 2020

Makombora yarushwa katika mji mkuu wa Eritrea


Wanadiplomasia wamesema makombora yamerushwa katika mji mkuu wa Eritrea, Asmara, wakati mapigano katika jimbo la kaskazini la Tigray yakionekana kuvuka mpaka hadi katika nchi jirani.Waangalizi wanasema mapigano hayo yamezua hofu na wasiwasi mkubwa. 


Takriban makombora matatu yalilenga uwanja wa ndege mjini Asmara, saa chache tu baada ya uongozi katika jimbo la Tigray kuonya kuwa unaweza kufanya mashambulizi.


Uongozi wa Tigray unaishtumu Eritrea kwa kuishambulia kutokana na mwaliko wa serikali ya Ethiopia, tangu vita katika jimbo hilo la kaskazini kuanza mnamo Novemba 4.Hata hivyo hakujatangazwa taarifa zozote za kutokea uharibifu au vifo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...