Search This Blog

Monday, November 9, 2020

Kiongozi wa Tigray aitaka AU kuingilia kati mzozo wa Ethiopia


Kiongozi wa jimbo la Tigray Kaskazini mwa Ethiopia ametoa wito kwa Umoja wa Afrika kuingilia kati mgogoro nchini humo usifikie hatua ya kuingia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Katika taarifa aliyoitoa kwa njia ya televisheni, Debretsion Gebremichael alisema Tigray itaendelea kujitetea mpaka pale serikali itakapokubali kufanya mazungumzo.

Lakini Waziri Mkuu wa Ethiopia , Abiy Ahmed, amesema kuwa vitendo vya viongozi wa Tigray vilivyovuka mpaka vimemfanya achukua hatua za kijeshi.

Ripoti kutoka mji jirani wa Amhara zinasema wanajeshi 100 wa serikali walikuwa wakipatiwa tiba ya majeraha.

Awali, Bwana Abiy bila kutoa maelezo amewafuta kazi mkuu wa jeshi, mkuu wa idara ya Intelijensia na waziri wa mambo ya nje

Mkuu mpya wa jeshi Berhanu Jula amesema kuwa vikosi vya serikali vimedhibiti miji minne Magharibi mwa Tigray.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...