Kiongozi wa jimbo la Tigray Kaskazini mwa Ethiopia ametoa wito kwa Umoja wa Afrika kuingilia kati mgogoro nchini humo usifikie hatua ya kuingia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Katika taarifa aliyoitoa kwa njia ya televisheni, Debretsion Gebremichael alisema Tigray itaendelea kujitetea mpaka pale serikali itakapokubali kufanya mazungumzo.
Lakini Waziri Mkuu wa Ethiopia , Abiy Ahmed, amesema kuwa vitendo vya viongozi wa Tigray vilivyovuka mpaka vimemfanya achukua hatua za kijeshi.
Ripoti kutoka mji jirani wa Amhara zinasema wanajeshi 100 wa serikali walikuwa wakipatiwa tiba ya majeraha.
Awali, Bwana Abiy bila kutoa maelezo amewafuta kazi mkuu wa jeshi, mkuu wa idara ya Intelijensia na waziri wa mambo ya nje
Mkuu mpya wa jeshi Berhanu Jula amesema kuwa vikosi vya serikali vimedhibiti miji minne Magharibi mwa Tigray.

No comments:
Post a Comment