Search This Blog

Wednesday, November 11, 2020

Katibu Mkuu wa Shirika la Ukombozi wa Palestina aliyefariki kwa corona azikwa


Katibu Mkuu wa Halmashauri ya Shirika la Ukombozi wa Palestina (PLO), Dk. Saeb Erekat amefanyiwa mazishi ya safari yake ya mwisho.

Shughuli ya mazishi ya Erekat ambaye alifariki hospitalini alipokuwa akifanyiwa matibabu baada ya kukutwa na virusi vya corona (covid-19), ilifanyika katika Ukingo wa Magharibi.

Mwili wa Erekat uliokuwa ukihifadhiwa hapo jana katika hospitali ya Hadassah iliyoko Jerusalem ya Magharibi ya Israel, ulisafirishwa leo hii hadi Ukingo wa Magharibi kwa ajili ya shughuli ya mazishi iliyoandaliwa mjini Ramallah na mamlaka ya rais wa Palestina.

Shughuli hiyo ya mazishi ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa ngazi za juu za serikali ya Palestina akiwemo Rais Mahmud Abbas na Waziri Mkuu Muhammed Ishtiyya.

Baada ya shughuli ya mazishi, jeneza la Erekat lilisafirishwa hadi mji wa Eriha kutoka Ramallah.

Mwili wa Erekat uliswaliwa katika msikiti wa Tarihi Eriha ambapo maelfu wa wananchi wa Palestina walijumuika.

Baadaye mwili wa Erekat ukasafirisha kutoka msikitini na kuzikwa katika eneo la makaburi ya Al-Babayi mjini Eriha.

 Erekat ambaye aliwahi kufanyiwa upandikizaji wa mapafu mwaka 2017 nchini Marekani, alikuwa na covid-19 tarehe 8 Novemba.

Baada ya hali yake afya kuwa mbaya, Erekat alisafirishwa tarehe 23 Oktoba kutoka kwenye nyumba yake mjini Eriha, Ukingo wa Magharibi na kulazwa katika hospitali ya Hadassah iliyoko Jerusalem Magharibi ya Israel.

Halmashauri ya Harakati ya Ukombozi wa Kitaifa wa Palestina ilitoa maelezo hapo jana na kutangaza Erekay alifariki katika hospitali aliyokuwa akitibiwa.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...