Search This Blog

Sunday, November 1, 2020

Dkt. Magufuli akabidhiwa cheti, aipongeza tume kwa hili

Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli, leo Novemba 1, 2020, amekabidhiwa cheti cha ushindi wa nafasi hiyo na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji mstaafu Semistocles Kaijage.

Hafla hiyo ya kukabidhiwa cheti cha ushindi, imefanyika jijini Dodoma ambapo kabla ya kukabidhi, Jaji Kaijage alisema uchaguzi ulienda vizuri kuanzia Oktoba 28 zoezi la upigaji kura lilipoanza, hadi Oktoba 30, alipotangazwa mshindi wa urais.

Aidha Jaji Kaijage pia amemkabidhi cheti cha ushidni Makamu wa Rais mteule ambaye ni Samia Suluhu Hassan.


Baada ya kukabidhiwa cheti hicho, Magufuli ameishukuru tume kwa kuendesha uchaguzi wa huru na haki pamoja na kufanikisha kukamilika kwa zoezi hilo mapema.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...