Hafla hiyo ya kukabidhiwa cheti cha ushindi, imefanyika jijini Dodoma ambapo kabla ya kukabidhi, Jaji Kaijage alisema uchaguzi ulienda vizuri kuanzia Oktoba 28 zoezi la upigaji kura lilipoanza, hadi Oktoba 30, alipotangazwa mshindi wa urais.
Aidha Jaji Kaijage pia amemkabidhi cheti cha ushidni Makamu wa Rais mteule ambaye ni Samia Suluhu Hassan.
Baada ya kukabidhiwa cheti hicho, Magufuli ameishukuru tume kwa kuendesha uchaguzi wa huru na haki pamoja na kufanikisha kukamilika kwa zoezi hilo mapema.


No comments:
Post a Comment