Search This Blog

Thursday, November 12, 2020

Askari wanaodaiwa kumuua mwanachama wa ACT wakamatwa

 

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja linawashikilia watu saba kwa tuhuma za mauaji ya Said Salum Suleiman (32) mkazi wa Mwembemakumbi mjini Unguja.

Wanaoshikiliwa kwa tuhuma za mauaji ya Suleiman ambaye alikuwa Katibu wa ACT-Wazalendo Tawi la Mwembemakumbu ni Askari wanne wa Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na Maofisa watatu wa idara ya misitu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Awadh Juma Haji amesema Suleiman alipigwa risasi na Maofisa hao eneo la Mwembemakumbi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...