Search This Blog

Thursday, October 1, 2020

UEFA wameruhusu mashabiki viwanjani


UEFA wametangaza kuwa wataruhusu mashabiki kuingia uwanjani katika mechi za Champions League na timu ya taifa kwa asilimia 30 ya uwezo wa uwanja kuchukua mashabiki.

Uamuzi huo utatekelezwa endapo sheria za taifa husika hazitakuwa zinazuia, kingine katika michezo hiyo mashabiki wa timu mgeni hawatoruhusiwa kuingia viwanjani kama tahadhari ya Corona.

Hii ni ishara njema na inakuja ikiwa ni miezi takribani saba toka michezo isimame na mashabiki kutoruhusiwa kuingia viwanjani kutokana na kuingia kwa virusi vya Corona katika mataifa ya Ulaya mwezi March 2020.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...