Search This Blog
Tuesday, October 20, 2020
Sudan kuondolewa kwenye orodha ya wafadhili wa makundi ya kigaidi
Rais wa Marekani Donald Trump amesema ataiondoa Sudan katika orodha ya wafadhili wa ugaidi iwapo italipa fidia ya dola milioni 335 (£259m).
Waziri mkuu wa Sudan Abdalla Hamdok amejibu kuwa fedha hizo zimeshatolewa tayari lakini hakukuwa na majibu ya haraka kutoka Marekani.
Sudan imekuwa katika orodha ya wafadhili wa ugaidi tangu mwaka 1993 wakati kiongozi wa al-Qaeda Osama Bin Laden alipoishi huko kama mgeni wa serikali.
Fidia hiyo inahusisha mabomu yaliolipuliwa na al-Qaeda mwaka 1998 katika balozi za Marekani barani Afrika.
Shambulio hilo lililotokea Tanzania na Kenya lilouwa watu zaidi ya 220 na fidia hiyo inapaswa kulipwa kwa wahanga na familia za waliopoteza ndugu zao", bwana Trump alisema.
Uhusiano wa Marekani na Sudan umeimarika tangu rais Omar al-Bashir alipoweza kukabiliana na maandamano makubwa mwaka jana na hatimaye kuondolewa madarakani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment