Search This Blog

Thursday, October 22, 2020

Mpenzi wa Duma achezea kichambo kwa watanzania



Mpenzi wa msanii wa filamu Duma Actor aitwaye Mishi Dorah amesema amechambwa sana na watu kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuonyesha kuwa yupo kwenye mahaba mazito na msanii huyo wa filamu.

Mishi Dorah ambaye anatokea Nairobi,Kenya amesema hachoshwi na kelele za watu wa Instagram kwani hazimuumizi kichwa na sasa hivi wapo kwenye mahusiano  kwa miaka mitatu na anaenjoy kuwa na Duma Actor.


"Duma ni 'Gentleman' na ndiyo mwanaume wa ndoto zangu, nilitamani kuwa naye na mtu mzuri sana kwangu, tayari nimeshafika kwao ila nimegundua kuna mawifi wengi na wanachamba sana ila nime-enjoy" amesema Mishi Dorah


Aidha kwa upande wa Duma Actor amesema "Mimi sifanyi kiki kuhusu kupost mitandaoni kama tupo kwenye mahusiano, huyu ni mchumba wangu na mke wangu mtarajiwa, mahusiano yetu yana zaidi ya miaka mitatu tulivyokutana damu zetu zikaendana"



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...