Search This Blog

Sunday, October 18, 2020

Michael Gove wa Uingereza asema wamejiandaa kwa Brexit bila makubaliano

 


Waziri anayeshughulika na mkataba wa kujiondoa kwa Uingereza katika Umoja wa Ulaya almaarufu Brexit, Michael Gove, amesema leo kwamba Uingereza ''imejiandaa vizuri'' kwa kuondoka katika Umoja huo bila ya mkataba. 

Katika nakala kupitia jarida la Sunday Times , Gove amesema kuwa hali hiyo sio anayopendelea lakini kama chaguo ni kati ya mpangilio unaowafunga kwa muda usiojulikana ama pale wanapoweza kujipangia mwelekeo wao wa siku zijazo, basi hakuna chaguo hapo. 

Ameongeza kuwa kuondoka kwa matakwa ya Australia ni matokeo ambayo wamejipanga nayo.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...