Search This Blog

Saturday, October 31, 2020

Marekani yafanya majaribio ya kombora lenye uwezo wa kubeba nyuklia na kusafirisha angani



Mamlaka ya Jeshi la Anga nchini Marekani imetangaza kufanya majaribio hapo jana ya kombora aina ya "Minuteman III" linaloweza kubeba nyuklia na kusafirisha angani.

Kwa mujibu wa maelezo yalitolewa na mamlaka hiyo, iliarifiwa kuwa kombora hilo lililojaribiwa kwenye kambi ya jeshi la anga ya Vandenberg iliyoko California, halikubebeshwa nyuklia wakati wa majaribio.


Maelezo zaidi yalibainisha uwezo na nguvu kubwa ya kijeshi iliyokuwa nayo Marekani, na kuthibitisha kuwa tishio kwa kipindi hiki cha karne ya 21.


Chombo cha kilichotumiwa kubeba kombora hilo hewani, kilisafiri kwa masafa ya maili 4,200 angani hadi kufikia kisiwa cha Kwajelin.


Mamlaka ya jeshi pia iliweza kuchapisha picha za urushaji wa kombora hilo katika mtandao wa kijamii.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...