Search This Blog

Sunday, October 4, 2020

Maofisa watano wa polisi wafukuzwa kazi kwa tuhuma za kuharibu ushahidi wa tukio la ubakaji India


Maofisa 5 akiwemo Kamanda wa Wilaya wameachishwa kazi wakituhumiwa kuharibu ushahidi wa tukio la binti wa miaka 19 kubakwa na kuuawa na kundi la wahuni jambo lililosababisha maandamano ya watu

Polisi hao wanatuhumiwa kuchelewesha usajili wa kesi pamoja na malalamiko ya ndugu wa marehemu na pia walifanya maamuzi ya kuuchoma mwili wa marehemu bila ridhaa ya familia yake

Aidha, Polisi wamekosolewa na jamii wakidaiwa kuvizuia Vyombo vya Habari na Vyama vya Siasa vya Upinzani kuongea na familia ya marehemu

Marehemu alifanyiwa ukatili huo na wanaume 4 katika eneo lililo karibu na kijiji alichokuwa anaishi Kaskazini mwa #India




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...