Rais wa World Bank, David Malpass amesema janga la #CoronaVirus linaweza kusababisha changamoto ya kulipa madeni katika baadhi ya nchi
Amesema, wawekezaji wawe tayari kutoa misaada ambayo inaweza kujumuisha kufutwa kwa madeni hayo kwani ni dhahiri nchi nyingine haziwezi kulipa fedha ambazo zimechukua
Mwezi Agosti, Malpass alionya mlipuko huo unaweza kuwapeleka watu Milioni 100 katika umasikini. Ametoa wito kwa Benki Binafsi na Mashirika ya Uwezekaji kujihusisha zaidi katika suala hilo

No comments:
Post a Comment