Search This Blog

Thursday, October 15, 2020

BAKWATA: Viongozi wa dini wasifanye kampeni kwenye nyumba za Ibada



Baraza za Ulamaa BAKWATA Taifa chini ya Mwenyekiti, Mufti Sheikh Abubakar Zubeir Mbwana ambaye pia ni Sheikh Mkuu wa Tanzania limetoa maelekezo kutokana na yanayojitokeza katika Kampeni za Uchaguzi Mkuu

Limewasihi Viongozi wa Dini kubaki kuwa wasuluhishi na wapatanishi wa jamii inayowahusisha wafuasi wa vyama na wasio na vyama

Pia limewataka Viongozi wote wa Baraza kutofanya Kampeni, hasa katika nyumba za ibada, na wanaoenda kinyume na mafundisho ya Uislamu na maadili ya BAKWATA watachukuliwa hatua za kinidhamu

Aidha, limewataka Waislamu kuiombea nchi ili Uchaguzi Mkuu upite salama na kwa amani



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...