Mevlüt Çavuşoğlu waziri wa mambo ya nje wa Uturuki atarajiwa kufanya ziara rasmi katika ukanda wa Afrika Magharibi.
Ziara yake hiyo waziri wa mambo ya nje wa Uturuki atajielekeza nchini Mali, Senegal na Guinea Bisau.
Ziara hiyo ya waziri wa mambo ya nje wa Uturuki itachukuwa muda wa siku tatu kuanzia Septemba 9 hadi Septemba 11.
Masuala tofuati katika ushirikiano uliopo kati ya Uturuki na mataifa hayo katika ukanda wa Afrika Magharibi yatajadiliwa.
Taarifa iliotolewa na wizara ya mambo ya nje ya Uturuki imefahamisha kwamba suala zima kuhusu uwekezaji, usalama ushirikiano wa kidiplomasia na maendelea CEDEAO ndio masuala muhimu ambayo yatazungumziwa katika ziara ya awaziri wa mambo ya nje wa Uturuki na viongozi tofauti katika Ukanda huo.
Imearifiwa kuwa ziara ya waziriwa mambo ya nje wa Uturuki nchini Senegal na Ginea Septemba 10 ndio itakuwa ziara yake ya kwanza katika mataifa hayo kama waziri wa mambo ya nje.
Masuala tofauti ya ushirikiano kati ya Uturuki na mataifa hayo pia yatajadiliwa ikiwemo pia masuala ya kimataifa.

No comments:
Post a Comment