Search This Blog
Sunday, September 13, 2020
Uganda kufungua uwanja wa ndege wa Entebbe
Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Uganda (UCAA), inatarajia kufungua uwanja wa kimataifa wa Entebbe na kuruhusu safari za ndani na nje, Kuanzia Oktoba 1, mwaka huu, baada ya miezi mitano ya kuzuia safari za ndege za abiria ili kudhibiti maambukizi ya Covid 19.
Hatua hiyo ni mfululizo wa jitihada za Serikali ya nchi hiyo chini ya rais Yoweri Museveni, kulegeza masharti, na kufufua uchumi ulioathirika vibaya kutokana na mlipuko wa ugonjwa huo.
Aidha mamlaka hiyo imesema kuwa ndege 13 zimeruhusiwa kuingia na kutoka kwa siku ya kwanza na 10 zitafanya safari siku ya pili.
Miongoni mwa mashirika yanayotarajiwa kufanya safari ni pamoja na Uganda Airlines, Air Tanzania, Kenya Airways, Emirates, RwandAir na KLM.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment