Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TANESCO, Dkt. Alexander Kyaruzi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) litachochea kasi ya ukuaji wa viwanda mkoani Simiyu kwa kujenga kituo kipya cha kupoza na kusambaza Umeme wa takriban megawati 90 katika eneo la Imalilo, Bariadi Mkoani Simiyu. Mkoa huo kwa sasa una takribani Megawati 10.
Dkt. Kyaruzi ameeleza kuwa, ujenzi wa kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Imalilo Bariadi chenye uwezo wa kusambaza takriban Megawati 100, kitajengwa sambamba na njia ya kusafirisha umeme toka Shinyanga yenye urefu wa kilomita 109.

No comments:
Post a Comment