Search This Blog

Saturday, September 12, 2020

TANESCO kuchochea kasi ya ukuaji viwanda

 


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TANESCO, Dkt. Alexander Kyaruzi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) litachochea kasi ya ukuaji wa viwanda mkoani Simiyu kwa kujenga kituo kipya cha kupoza na kusambaza Umeme wa takriban megawati 90 katika eneo la Imalilo, Bariadi Mkoani Simiyu. Mkoa huo kwa sasa una takribani Megawati 10.

Dkt. Kyaruzi ameeleza kuwa, ujenzi wa kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Imalilo Bariadi chenye uwezo wa kusambaza takriban Megawati 100, kitajengwa sambamba na njia ya kusafirisha umeme toka Shinyanga yenye urefu wa kilomita 109.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...