Safari za ndege kati ya Uturuki na Yordani zaanza upya n baada ya kusitishwa kutokana na maambukizi ya virusi vya corona.
Kama mataifa mengine ulimwenguni yalivyofanya kwa ajili ya kuzuia maambukizi ya virusi vya corona, Uturuki pia ilifunga mipaka yake na mataifa mengine ulimwenguni.
Safari ya kwanza ya abiria na biashara kati ya Uturuki na Yordani imefanyika kati ya jiji la Istanbul na jiji la Amman.
Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Amman umeanza kupokea ndege kutoka nchini Uturuki baada ya kutangazwa kufunguliwa safari za ndege.
Ndege ya shirika la ndege şa Uturuki la THY imewasili katika uwanja wa ndege wa Amman majira ya usiku Jumanne.
Safari ya mwisho kati ya Uturuki na Yordani ilifanyika Machi 17.

No comments:
Post a Comment