Search This Blog

Sunday, September 6, 2020

Rais Erdogan azidisha cheche za maneno kwenye mvutano na Ugiriki

Rais wa Uturuki Reccep Tayyip Erdogan, ameionya Ugiriki kuingia katika mazungumzo kuhusu eneo linalozozaniwa la mashariki mwa bahari Mediterrania, au waathiriwe.

Akizungumza katika hafla ya kufungua hospitali mjini Istanbul, Erdogan amesema, Ugiriki italazimika kuelewa lugha ya siasa na diplomasia au uwanjani kwa madhara machungu.

Uturuki inazozana na Ugiriki pamoja na Cyprus kuhusu haki za kutafuta gesi na mafuta mashaeriki mwa bahari Mediterrania.

Pande zote kwenye mvutano huo zimepeleka vikosi vya jeshi vya majini na angani kutetea madai yao katika eneo hilo.

Hayo yakijiri, gazeti la Cumhuriyet la Uturuki limeripoti kuwa vifaru 40 vya kijeshi vimekuwa vikisafirishwa kutoka mpaka wa Syria kuelekea Edirne, kaskazini magharibi mwa Uturuki.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...