Search This Blog
Wednesday, September 9, 2020
Mtandoa wa TikTok uko mbioni kuondoa VIDEO ya mtu aliyekuwa akijitoa uhai
Matandao wa kijamii wa TikTok unajitahidi kuondoa kanda ya video inayomuonesha mtu akijjitoa uhai. Video hiyo ambayo imekuwa ikisambazwa kwenye mtandao huo kwa siku kadhaa, ilianzia kwenye Facebook na sasa imeanzakusambazwa Twitter na Instagram.
TikTok ni maarufu kwa vijana wadogo – na baadhi yao wameripotiwa kutazama video hiyo na wamepata usumbufu wa kimwazo.
Mtandao huo umesema utawapiga marufuku akaunti za watu watakaoendelea kusambaza video hiyo mara kadhaa.
”Tunawashukuru wafuatiliaji wa mtandao wetu ambao wameripoti kuhusu video hiyo na kuwatahadharisha wengine dhidi ya kuitazama ama kushirikisha maudhui kama hayo kwenye jukwaa lolote, kwa heshima ya mtu huyo na familia yake” mwakilishi wa TikTok alisema.
Kwa upande wake Facebook imeiambia BBC: “Tulifuta video hiyo mwezi uliopita kwenye mtandao Facebook, siku iliyooneshwa moja kwa moja, na kutumia mfumowa teknolojia kufuta nakala za video zinazochapishwa kutoka wakati.
“Tunatoa pole zetu kwa familia ya Ronnie na marafiki wakati huu mgumu.”
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment