Search This Blog

Thursday, September 17, 2020

"Israeli inapaswa kushtakiwa katika Mahakama ya Uhalifu ya Kimataifa"- Canada


Wananchi wa Canada wanahisi kuwa Israeli inapaswa kushtakiwa katika Korti ya Uhalifu ya Kimataifa kwa uhalifu wake wa kivita.

Matokeo ya uchunguzi uliofanywa na mashirika 3 yasiyo ya kiserikali kwa Utafiti wa EKOS yamechapishwa, ripoti hiyo ikiwa na kichwa cha habari,"Hakuna Upendeleo: Wananchi wa Canada Wanatarajia kutopendelewa kabisa kwa Israeli".

Kulingana na ripoti hiyo, asilimia 84 ya wahojiwa walisema kuwa Israeli inapaswa kushtakiwa katika Korti ya Uhalifu ya Kimataifa (ICC) kwa uhalifu wa kivita na ukiukaji wa haki za binadamu.

Ripoti hiyo pia imesema kwamba asilimia 86 ya wananchi wa Canada wamepinga nchi yao kupuuza ukiukaji wa haki za binadamu za Israeli kwa sababu tu ni mshirika wake.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...