Mtangazaji maarufu wa kipindi cha Ala za Roho cha Clouds FM, Diva the Boss ametangaza rasmi kuacha kazi katika kituo hicho baada ya kukitumikia kwa miaka 11 mfurulizo.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diva ameandika; “Mashabiki wangu wa #AalaZaRoho mambo vipi? Mimi mwenyewe kwa akili zangu binafsi maamuzi yangu binafsi nachukua nafasi hii kuwaaga, nitawa-miss sana.
“Tumekuwa wote kwa miaka 11, worth it, natoa shukran zangu kwa uongozi wa Clouds FM kwa kunilea, Im forever thankful, shukrani kwa Joseph Kusaga na familia yake for making My Journey, ntakushukuruni sana.
“Positively nimeamua mwenyewe kuacha kazi Clouds FM leo (jana) mchana huu kwa mdomo wangu mbele ya HR na shahidi wake nilipotamka maneno hayo ya maamuzi ambayo toka natoka nyumbani nilisema nitafanya sababu ya vitu vingi tu ambavyo sitasema.
“Nashukuru sana sana sana, I’v been raised to be honest and speak up no matter what, sababu ya kusimamia ukweli wangu nimeamua fanya maamuzi ambayo nahisi ni sahihi kwangu… By saying That Life has a lot to offer Mungu yu Mwema… tutajuzana zaidi my next destination, love You all 💕,” ameandika Diva.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment