Wizara ya mambo ya ndani ya Uturuki imefahamisha kwamba askari mmoja amefariki katika shambulizi la kigaidi lililoendeshwa na magaidi katika eneo la Hakkari.
Mkabiliano kati ya magaidi na wanajeshi wa Uturuki yalizuka baada ya magaidi kujaribu kuwavamia wanajeshi katika eneo hilo ambapo kumeanzishwa operesheni ya Yıldırım-1 Cilo.
Operesheni hiyo imeanzishwa na jeshi la Uturuki kwa lengo la kuwaondoa magaidi katika mipaka ya Uturuki kama ilivyoendeshwa operesheni nyingine mipakani mwa Uturuki.
Jeshi la Uturuki kwa uapande wake pia limefahamisha kuwaangamiza magaidi wawili .
Magaidi hao wameangamizwa wakiwa katika handaki lao ambalo walikuwa wakitumia kama maficho Yüksekova.

No comments:
Post a Comment