Search This Blog

Monday, September 21, 2020

Aliyeshukiwa kutuma barua yenye sumu kwenda Ikulu ya Marekani akamatwa


Mwanamke mmoja amekamatwa akishukiwa kutuma kifurushi kilicho na sumu aina ya ricin kwenda kwa Rais wa Marekani,Donald Trump.Maafisa wa uhamiaji wa Marekani wameeleza.

Mwanamke huyo ambaye hajatajwa jina alikamatwa kwenye mpaka huko Buffalo, New York , akijaribu kuingia Marekani akitokea Canada, na anaripotiwa kukamatwa akiwa na silaha.

Barua iliyokuwa na sumu kali inaaminika kutoka nchini Canada, kwa mujibu wa wapelelezi.

Barua iligundulika juma lililopita kabla ya kufika ikulu ya Marekani.

Ricin huzalishwa kutoka kwa usindikaji wa maharagwe ya castor, mmea katika familia ya Euphorbiaceae. Mbegu zake hutumiwa kutengeneza sumu.

Ni sumu hatari, ambayo kumeza, kuvuta harufu yake au kudungwa sindano, kunaweza kusababisha kichefu chefu, kutapika, kutokwa na damu ndani mwili na kuzuia viungo muhimu vya ndani kukosa kufanya kazi na hatimaye kifo.

Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) na maafisa wa ulinzi wa siri wanachunguza barua hiyo ilitumwa kutoka wapi na ikiwa kuna nyengine zilitumwa kupitia huduma za posta za Marekani.

"Kwa sasa hakuna tishio linalojulikana kwa usalama wa umma ," FBI iliambia CNN katika taarifa siku ya Jumamosi.

Mshukiwa huyo anashukiwa kuwa huenda alituma sumu hiyo pia huko Texas, kwenye gereza na ofisi ya maafisa wa polisi.Taarifa ya Shirika la habari CNN limeeleza.

Idara ya polisi nchini Canada ilisema siku ya Jumamosi kuwa inashirikiana na FBI kuchunguza barua hiyoiliyotumwa kwenda Ikulu ya Marekani.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...