Search This Blog

Sunday, August 23, 2020

Wajumbe kutoka Afrika Magharibi wakutana na wanajeshi waliomwondoa madarakani rais Ibrahim Keita

Viongozi waandamizi kutoka nchi za Afrika magharibi wamekutana na wanajeshi waliomwondoa madarakani rais Ibrahim Boubacar Keita.

Ujumbe huo pia ulikutana na rais huyo aliyepinduliwa. Juhudi za kusuluhisha zilianza kufanywa baada ya maalfu ya wananchi wa Mali kujitokeza katika mji mkuu Bamako ili kuunga mkono hatua iliyochukuliwa na wanajeshi.

Viongozi hao kutoka nchi za jirani wanafanya mazungumzo kwa lengo la kuurejesha utawala wa kiraia nchini Mali.

Jumuiya ya nchi za Afrika Magharibi, ECOWAS imelaani vikali kuangushwa kwa rais huyo na imesema itafanya juhudi ili kurejesha haraka utawala ulio katika msingi wa katiba na pia imesema inataka rais aliyepinduliwa Ibrahim Boubacar Keita arudishwe madarakani mara moja.

Jumuiya ya kimataifa pia imeleezea wasi wasi juu ya kuangushwa kwa rais Keita. Kiongozi wa ujumbe huo wa nchi za Afrika magharibi, Goodluck Jonathan aliyekuwa rais wa Nigeria amesema Keita anaendelea vizuri.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...