Search This Blog
Saturday, August 29, 2020
Usiogope Kuambiwa Unajipendekeza Sana, Ki Kubwa Jipendekeze Kwa Malengo
Siku zote huwa kuna watu ambao kazi yao kubwa ni kama mawakala wa shetani kwa hiyo huwaga wanatumia mbinu mbalimbali kukudhoofisha pale ambapo wanaona kuna dalili ya wewe kupiga hatua flani.
Na wengi wanaweza kukuambia hili neno UNAJIPENDEKEZA sio kwamba kweli wana maanisha hapana wanasema hivyo kwa sababu huenda mtu uliye naye karibu nao wanatamani wangekuwa na nafasi hiyo sasa ili kujikinga wanatumia mgongo wa neno KUJIPENDEKEZA.
Siku zote katika maisha ili ufanikiwe unahitaji kuwa karibu na watu waliofanikiwa na ili uwe karibu na watu waliofanikiwa lazima ujenge ukaribu nao sana ili nao wapate nafasi ya kukujua ili waweze kukusaidia pale ambapo kuna jambo unahitaji.
Neno UNAJIPENDEKEZA litakuwa baya sana pale ambapo utakuwa unajiweka karibu na watu ili kuharibia watu flani jambo ambalo sio zuri hata kidogo ila kama unajipendekeza kwa sababu kuna mambo yako unataka yafanikiwe bila kuathiri mtu mwingine basi usitie hofu kabisa.
Msingi mkubwa wa watu waliofanikiwa walijiweka karibu sana na wale waliofanikiwa na wangekuwa wanaogopa kujiweka karibu na watu hao kwa woga wa kuambia wanajipendekeza huenda mpaka leo wasingefika walipofika.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment