Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni alikutana na wananchi hao katika kikao cha wazi na kufikisha maamuzi ya serikali kutokana na Mgogoro huo ambao katika kipindi chote hicho ulikuwa ukisababisha Vurugu na Uvunjifu wa Amani katika eneo hilo.
Katika Uamuzi wake Serikali kupitia Wizara ya Ardhi ilisema kuwa baadhi ya eneo hilo sasa litakuwa Chini ya Serikali na kutumika kwa ajili ya Ujenzi wa Hospitali, shule na Soko pamoja na Huduma nyingine za Kijamii.
Hata hivyo Uamuzi huo Ulipokelewa ndivyo sivyo na Wananchi hao huku baadhi yao wakionyesha wazi kukataa Fidia iliyotolewa na serikali lakini wengine wakisababisha Vurugu na maneno yasiofaa kwa Mkuu wa Wilaya na kusababisha baadhi yao kukamatwa.
Hata hivyo Bi. Msafiri aliwasihi wakazi hao kuwa hakutakuwa na Mabadiliko katika Maamuzi hayo ya Serikali kinyume chake waende Mahakamani ingawa hukumu ya awali ilionyesha kuwa wananchi hao waliuza na kulitoa kwa hiari yao eneo hilo kwa Mwekezaji.
No comments:
Post a Comment