Search This Blog
Wednesday, August 26, 2020
Sakata la Messi Ngoma Nzito atajwa kuibukia inter Milan
KLABU ya Inter Milan ya Italia inatajwa kuwa miongoni mwa timu kutoka nchini humo ambazo zinapigania saini ya mshambuliaji wa FC Barcelona, Lionel Messi.
Rais wa zamani wa Inter Milan, Massimo Moratti anaamini kwamba klabu za Ligi Kuu Italia ‘Serie A’ zinajaribu kupigania saini ya mshambuliaji wa Kiargentina, Lionel Messi kutoka Barcelona hata kama hakuna uwezekano wa kutua huko.
Kwa mujibu wa Moratti ni kwamba Inter Milan ‘Nerazzurri’ ni miongoni mwa klabu hizo ambazo zipo kwenye vita ya kumnasa nyota huyo kufuatia kuonyesha kwake dhamira ya kutaka kuondoka Camp Nou.
Moratti ambaye alikuwa Rais wa Inter kati ya 1995 na 2013, anafikiri kwamba tangazo la hivi karibuni ambalo lilionekana katika runinga likifanywa na wamiliki wa klabu hiyo kwenye kanisa kuu la Milan la Duomo ni ishara kwamba wako tayari kumleta San Siro.
“Sio operesheni rahisi kiuchumi, hiyo ni wazi. Lakini kizuizi kikubwa ni nia ya Messi. Lazima uelewe ikiwa anataka kutoka Barca kabisa.
“Nadhani Inter Milan tayari wamejaribu [kutaka kumsajili]. Nimeona tangazo hili linanifanya nifikirie kwamba pengine tayari kuna mpango umesukwa wa kuhakikisha anasajiliwa. Kama sivyo, nadhani watafanya hivi karibuni,” Moratti aliiambia AS
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment