Search This Blog

Saturday, August 29, 2020

Rais wa Uturuki ampokea mkuu wa baraza kuu la Libya



Halid al Mashri, mkuu wa baraza  kuu la Libya katika ziara yake nchini Uturuki amepokelewa na rais Recep Tayyıp Erdoğan  mjini Istanbul.

Halid al Mashri  amewasili Uturuki Alkhamis ambapo amefanya mazungumzo na rais Erdoğan na viongozi wengine wa ngazi za juu wa Uturuki.

Katika mazungumzo yao , viongozi hao wa wamejadili kuhusu masuala tofauti kuhusu ushirikiano kati ya Uturuki na Libya.

Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Mevlüt Çavuşoğlu amezungumza pia na  Halid al Mashri.

Katika ujumbe wake aliotoa katika ukurasa wake wa Twitter, waziri wa mambo ya nje wa Uturuki amesema kwamba  ushirikiano kati ya Uturuki na Libya unazidi kuimarika siku hadi siku.

Katika mazungumzo yao viongozi  hao wamezungumzia pia kuhusu ushirikiano katika sekta ya uchumi na biashara na ulinzi.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...