Search This Blog
Saturday, August 22, 2020
Polisi Wazungumzia Ajali iliyoua 8 na Kujeruhi 27
Watu Nane wamefariki Dunia na wengine 27 wamejeruhiwa, baada ya Basi la Sabuni Express lililokuwa likitoka Wilaya ya Muleba mkoani Kagera kuelekea mkoani Mwanza kupinduka katika kijiji cha Lutenge kilichoko wilayani Muleba.
Akizungumza na East Africa Television Kamanda wa Polisi Mkoani Kagera Revocatus Malimi, amesema kuwa marehemu sita kati ya nane wamekwishatambuliwa na ndugu zao na kuwa miili yao imehifadhiwa katika Hospitali za Rubya na Ndolage zilizoko katika Wilaya hiyo.
Kamanda Malimi amesema kuwa chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika, ambapo ametaja majina ya marehemu waliotambulika na ndugu zao kuwa ni Justus Ruhoya, Philbert Katabazi, Paskazia Pastory, Vestina Clonery, Goleth Adolph na Prisca Revocatus ambaye ni mtoto wa mwezi mmoja, wote wakazi wa Wilaya ya Muleba.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment