Search This Blog
Wednesday, August 5, 2020
Polepole Awaka ”CHADEMA waombe radhi kubadili wimbo wa Taifa”
Katibu wa uenezi wa chama cha mapinduzi (CCM) Humprey Polepole ameshangazwa na kitendo cha chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) kubadilisha beti kwenye wimbo wa taifa wakati wa mkutano mkuu wa chama hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 5, 2020 Jijini Dar es Salaam katika ofisi ndogo za chama hicho Lumumba amesema kitendo cha chama hicho kubadilisha nyimbo hiyo ni kuvunja sheria.
“Hiki nichama ambacho kabla hakijapata dola kinaanza kubadilisha wimbo wa watanzania kuwa wimbo wa chama chao, tena kwa kujimwambafai kuwa wako sahihi, huu ni wimbo unowatambulisha watanzania sio wimbo unaotambulisha chama cha mtu fulani” amesema Polepole.
“Mimi hiki Chama nimeshindwa kukielewa, nidhamu ni zero, kutii sheria bila shuruti ni zero, kama haikutosha ikaja ya wimbo wa Taifa, bila aibu wanajenga hoja tuambieni wapi tunavunja sheria”amesema Polepole
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment