Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi, Dk Wilson Mahera amesema tume bado haijatoa taarifa yoyote ya kutangaza mgombea wa mbunge au Udiwani ambaye amepitishwa bila kupingwa.
" Kwa mujibu wa kifungu cha 40 (2) cha sheria ya Tume ya Uchaguzi sura ya 343 pingamizi linaweza kuwekwa kwa wagombea wa ubunge kama zuio kwa wagombea aliyeteuliwa kuanzia saa kumi jioni ya siku ya uteuzi hadi saa kumi jioni ya siku inayofuatia baada ya siku ya uteuzi” Dk Mahera amesema

No comments:
Post a Comment