Search This Blog
Monday, August 24, 2020
Dkt Louis Shika "900 itapendeza", afariki dunia
Habari kutoka kijiji cha Nyanguge Wilayani Magu Mkoani Mwanza zimethibitisha kufariki kwa Dkt Louis Shika ambaye alijipatia umaarufu mitandaoni baada ya kutangaza kutaka kununua nyumba za mnada huko Kigamboni kwa Shilingi Milioni 900.
Ndugu wa karibu wa marehemu amesema ni kweli Dkt Shika alilazwa Katika Kituo cha Afya Nyanguge wilaya ya Magu mkoani Mwanza kwa siku kadhaa akipatiwa matibabu baada ya kuugua kwa muda mrefu lakini baadaye alitolewa hospitali na kurudishwa nyumbani ambapo umauti umemfika jana .
Aidha wamesema taratibu za mazishi zinaendelea na kuna uwezekano mkubwa akazikwa leo Agosti 25, 2020 kijijini hapo.
Ikumbukwe tu kipindi cha nyuma zilitoka taarifa kwamba Dkt Louis Shika anahitaji msaada wa kifedha kwa ajili ya kufanyiwa matibabu kwa sababu alikuwa anasumbuliwa na matatizo ya kiafya.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment